Na, John Kabambala:
Mimba za utotoni ni suala la kijamii na afya linaloathiri wasichana duniani kote, ikiwa ni pamoja na Tanzania. Mimba za utotoni ni suala linalosababisha wasichana kukatisha masomo yao na kuathiri maendeleo yao ya kielimu na kijamii. Katika juhudi za kukabiliana na tatizo hili, Serikali ya Tanzania imechukua hatua kadhaa, ikiwa ni pamoja na kuruhusu wasichana walio pata mimba na kujifungua kuendelea na masomo yao. Hapa tutachunguza suala la mimba za utotoni na uamuzi wa serikali kuhusu kuruhusu wasichana hawa kuwarejesha shuleni kuendelea na masomo.
MIMBA ZA UTOTONI
TANZANIA:
Mimba za utotoni ni tatizo kubwa nchini Tanzania, na lina
athari kubwa kwa maendeleo ya wasichana. Sababu za mimba za utotoni ni pamoja
na ukosefu wa elimu ya Afya ya uzazi, umasikini, ndoa za utotoni, unyanyasaji
wa kijinsia, na upatikanaji mdogo wa huduma za afya ya uzazi. Kulingana na
Taarifa ya Hali ya Watoto Duniani ya mwaka 2021,
asilimia 27% ya wasichana nchini
Tanzania wanapata mimba kabla ya kufikisha umri wa miaka 18.
Mimba za utotoni zinaweka vikwazo vikubwa katika maendeleo
ya wasichana. Wasichana wengi wanaopata mimba wanakatishwa masomo yao, na mara
nyingi wanakumbana na unyanyapaa na ubaguzi wa kijamii. Hii inaweza kuwa na
athari za muda mrefu kwa wasichana hawa, ikiwa ni pamoja na kupoteza fursa za
kielimu na kiuchumi.
UAMUZI WA
SERIKALI WA KURUHUSU WASICHANA WALIO PATA MIMBA KUENDELEA NA MASOMO:
Mwishoni mwa mwaka 2021, Serikali ya Tanzania ilichukua hatua
za kurekebisha hali hii na kutoa fursa zaidi kwa wasichana walio pata mimba kuendelea
na masomo. Hata hivyo ikimbukwe kwamba mwaka 2017, Serikali ilipitisha sera
mpya inayoruhusu wasichana walio pata mimba kurudi shuleni baada ya kujifungua.
Uamuzi huu ulifanywa kwa lengo la kuhakikisha kwamba wasichana hao hawakatishwi
masomo yao na wanapata nafasi ya kuendelea na elimu yao.
Hatua hii ilionesha maana kubwa katika kuboresha hali ya
wasichana walio pata mimba. Nakuwapa fursa ya kuendelea na masomo yao na
kujenga mustakabali bora zaidi kwa maisha yao. Hata hivyo, kuna changamoto
katika utekelezaji wa sera hii, kama vile ubaguzi wa kijamii na unyanyapaa
dhidi ya wasichana walio pata mimba.
Kufuatia waraka huo wa Serikali ulioelekeza wanafunzi wa
kike waliopata ujauzito warejee shule katika mfumo rasmi baada ya kujifungua
wadau wa Elimu nchini waliipongeza Serikali kwa hatua hiyo. Lakini nikwa namna
gani mwendelezo wa program hii unaendelea na kuleta matokeo chanya kwa jamii.
Herriet Mkaanga,
mwanaharakati wa watoto wa kike na Mkurugenzi wa Shirika la My Health Foundation ambalo
limekua likipigania suala hili kwa muda mrefu, aliishukuru Serikali
kwa hatua hiyo na kutoa maoni yake kuwa wapatiwe Elimu ya saikolojia kabla ya
kurejeshwa Shule ili wakafanye vizuri zaidi.
Mkaanga pia wakati wa mahojiano yangu alisema juhudi
nyingine zinazotakiwa kuchukuliwa dhidi yao ni kuwezesha mazingira yao ya
kujifunzia ili wasiingie tena katika ushawishi wa kupata ujauzito ikiwemo,
kuwasaidia taulo za kike, vyakula kwa Shule zenye mabweni.
kwa mujibu wa Takwimu za Elimu ripoti ya Best 2020 ilieleza
jumla ya idadi ya wanafunzi wa kike 1,135
sawa na 0.7% walipata ujauzito
katika Shule za Msingi, ilhali shule za Sekondari walikua 5,398 sawa 5.5% mwaka
2019.
Aidha matukio ya Mimba za utotoni yaliyoripotiwa Ofisi ya
Afisa ustawi wa Jamii Mkoa wa Morogoro, yaliongezeka kutoka 800 mwaka 2019/2020
hadi kufikia zaidi ya 1200 Mwaka 2020/2021.
Akithibitisha Takwimu hizo Afisa usatawi wa Jamii Mkoa wa
Morogoro Bi, Jessica Kagunila, alisema sababu ya Mimba za utotoni kuongezeka
inachangiwa na Mila na Desturi za Mkoa huo pamoja na malezi yasiyo mazuri ya
watoto.
“Tukianza kwa
Mwaka 2019/2020 matukio ya mimba za utotoni yaliyoripotiwa ni 800 lakini tukija
kwa Mwaka 2020/2021 yameongezeka hadi kufikia zaidi ya 120, hii ni kutokana na
Mila na desturi na malezi yasiyo mazuri kwa upande wa walezi na wazazi’’
alisema Jessica Kagunila
Kwa mujibu wa Ofisi ya muendesha Mashtaka Mkoa wa Morogoro
DPP, matukio ya mimba za utotoni ambayo kisheria huitwa matukio ya ubakaji
yanaongezeka kutokana na watuhumiwa wa makossa hayo kutoa Rushwa kwa waathirika
na kesi kukosa ushahidi Mahakamani, alisema kaimu uendesha mashtaka wa Mkoa wa
Morogoro Flora Massawe.
“Inatokea mara
nyingi mahakamani, mashahidi wengi ambao ni wahanga watoto wanakuja kugeuka
yaani ule ushahidi waliotoa Polisi kwamba wamefanyiwa kitendoi cha ubakaji na
flani wakifika mahakamani wanakuja kukataa, na hii tumebaini kutokana na wazazi
kuridhia kufanya makubaliano na mtuhumiwa kuna kiasi cha Pesa wanalipana, basi
huku kesi zinaharibika’’ alisema Flora Massawe
Afisa ustawi wa Mkoa wa Morogoro Bi, Jessica Kagunila alieleza namna
ambavyo watazidi kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha matukio ya
Mimba na Ndoa za utotoni yanapungua.
Bi, Jessica alisema “Elimu sio suala la ustawi wa Jamii peke
yake, maendeleo ya Jamii na wadau wengine wa Elimu tutaendelea kushirikiana
kuzunguka shuleni kutoa elimu na hata kuwafikia wazazi kadri tutakavyoweza
pamoja na walimu ambao wanakaa muda mrefu na watoto’’
Katika kumulikia juhudi za Sekta binafsi kushirikiana na
Serikali juu ya kutokomeza Mimba za utotoni Mkoa wa Morogoro, Tanzania kids
time ilizungumza na Mratibu wa Miradi Evarist
Momburi, kutoka Shirika la SAWA WANAWAKE TAZNANIA lililojikita katika
kusimamia ulizi wa Mtoto na utoaji Elimu jumuishi kwa Shule za Msingi, ili
kusikia maoni yake pamoja na juhudi zao katika hili.
“kama tunataka
tupunguze hili tatizo la Mimba za utotoni, dawa yake ni kujenga mabweni na
kujenga Shule shikizi ambazo zitasaidia kupunguza ule umbali wa mwanafunzi
kutembea kuifata Shule ilipo, na hili tulifanya utafiti tukagundua watoto wengi
walikuwa wanakatiza masomo kwa sababu walikua wanapata changamoto ya umbali
kuifata Shule ilipo’’ Alisema
Evarist Momburi.
Alisema katika Mkoa wa Morogoro Shirika la, SAWA WANAWAKE
TANZANIA tayari limeshaboresha mabweni ya wasichana katika Shule za Sekondari
za DOMA na MVOMERO na Mwaka 2022 wamejipanga kuifikia Shule ya Sekondari WAMI
DAKAWA kupitia Mradi wake wa TUWALINDE WATOTO.
Kwa upande wake Bi,
Penina Sangiwa Afisa Elimu kutoka Shirika la umoja wa kimataifa la
kuhudumia watoto, alisema Serikali imepiga hatuka kubwa ya kuhakikisha kiloa
mtoto mwenye umri wa kusoma anapata Elimu, lakini bado kunajitihada
zinahitajika kuhakikisha lengo hilo linatimia.
Penina aliongeza kuwa ni jitihada kubwa zinatakiwa
kuchukuliwa na Serikali, wadau wa Elimu na mashirika na Taasisi mbalimbali
kueneza Elimu ya Afya ya uzazi kwa wasichana Shuleni ili kuepukana na mimba
ambazo zinaweza kujitokeza tena.
0 Comments